![]() |
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Katavi Makongoro Nyerere akiongoza kikao cha Kamati ya ushauri Mkoa wa Katavi |
Na Walter Mguluchuma-Katavi
Kamati ya ushauri ya
Mkoa wa Katavi (RCC) imepitisha mapendekezo ya rasmu ya
Bajeti ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Halmashauri zake tano
ya zaidi ya shilingi Bilioni 164
ikiwa imezingatia kuwaletea wananchi
maendeleo na kutatua kero
mbalimbali za wananchi .
Kamati ya ushauri ya Mkoa wa Katavi (RCC) imepitisha mapendekezo ya rasmu ya Bajeti ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Halmashauri zake tano ya zaidi ya shilingi Bilioni 164 ikiwa imezingatia kuwaletea wananchi maendeleo na kutatua kero mbalimbali za wananchi .
Mapendekezo hayo ya rasmu ya
bajeti yamepitishwa katika
kikao cha Kamati ya
ushauri ya Mkoa wa Katavi
kilichofanyika katika ikumbi wa ofisi ya
Mkuu wa huu kilichoongozwa na Kaimu
Mkuu wa Katavi Makongoro
Nyerere ambae pia ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa .
Akiwalisha mapendekezo
ya bajeti hiyo mbele ya wajunbe wa kikao Mtakwimu wa Mkoa wa Katavi Grace
Madaha amesema Ofisi ya
Mkuu wa Mkoa wa Katavi pamoja na Halmashauri zake zote tano za mkoa huu
wameomba kupitishiwa kwa
mwaka wa fedha wa 2025/ 2026 kiasi cha
shilingi Bilioni 164, 928,709,000
.
Amesema mapendekezohayo ya bajeti yamezingatia
vipaumbele mbalimbali ambavyo amevitaja kuwa ni kuinarisha
na kuboresha maeneo ya utawala
afya ,elimu na
umaliziahi wa miradi vipolo pamoja
na umaliziaji wa maboma 500 ya shule ambapo kila Halmashauri ya Mkoa huu inaidadi ya
maboma 100.
Ametaja vipaumbele vingine kuwa ni usimanizi wa mazingira ,mabadiliko ya
tabia ya nchi kwa
kuandaa mpango wa kuhifadhi
mazingira , kuwezesha wananchi
kiuchumi kupitia utowaji wa mikopo ya asilimia kumi kwa kupitia
mwongozo mpya wa
mwaka 2024 kwa vikundi vya wajasiriamali wanawake
vijana na watu wenye
ulemavu.
Madaha
amesema Pia wamepanga kutenga
fedha kwa ajiri ya kuilipa madeni
ya watumishi wazabuni na wakandarasi na kujenga
majengo ya utawala ya Halmashauri na nyumba za
baadhi ya watumishi ofisi ya mkuu wa
Mkoa na Halmashauri
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mpimbwe
Sailas Ilumba aliwasilisha
ombi la kuomba kutatuliwa
kwa migogoro ya mikapa kati ya wananchi wa
Halmashauri ya Mpimbwe na wananchi wa
Halmashauri ya Sumbawanga
Vijijini ,
Hivyo
amewataka viongozi wa
mikoa hiyo miwili
wasikubali kukaa na migogoro
kama hiyo ambayo inazungumzika hivyo
ameshauri kifanyike kikao cha pamoja
kuhadili swala hilo na kulitatua
kwa haraka sana .