MKOA WA KATAVI WATEKELEZA AGIZO LA RAIS KUHUSU LISHE

  

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko

Na  Walter  Mguluchuma

    Katavi.


Mkoa wa Katavi wamezindua  mpango   mkakati wa  kuondoa tatizo  la  udumamavu unao tokana na lishe   duni ikiwa ni  itekelezaji wa agiza  la Rais  alilolitokoa  mwaka 2024 kufatia  mkoa huo kuwa na idadi kubwa  ya watu  wemye udumavu .

 

Uzinduzi  huo wa  mpango wa kuondoa tatizo laudumavu  na lishe duni umezinduliwa rasmi na Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua  katika  ukumbi   wa Manispaa ya Mpanda na kuhudhuriliwa  na viongozi wa Mkoa   na  Wilaya zote za Mkoa wa wananchi ,viongozi  wa dini, kimila pamoja na wananchi mbalinbali  na  wahasiliamali .

 

Rc  Mrindoko amesema  kuwa  sote tunatambua  kuwa hali ya  udumavu  kwa watoto  chini  ya miaka  mitano   katika Mkoa wa Katavi  bado  ni changamoto  kubwa  kwa mujibu  wa takwimu  kuwango cha udumavu  katika Mkoa huu  ni asilimia  32.2 sawa na watoti  60,730 hali ambayo hairidhishi  kwani ipo juu  ya wastani  wa kitaifa  ambayo   ni asilimia  30.


Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mwanamvua Mrindoko akikagua baadhi ya mabanda wakati wa uzinduzi wa kampeni endelevu ya kupunguza udumavu unaosababishwa na lishe duni



Katika kukabiliana  na   changamoto hiyo ndio maana Mkoa huo umeweka  mikakati  mbalilimbali  kwa kuweza  kufanya uzinduzi  wa Kampeni   ya Mkoa ya kupambana  na  udumavu  kwa dhati  kabisa  kwenye  maeneo yote ya Mkoa huu .

 

Amebanisha kuwa  katika ziara yake aliyoifanya Rais Dkt Samia  Suluhu Hassan  mwaka hana kwenye  Mkoa huu aliwaagiza  viongozi wa Mkoa waende mkoa Njombe wakajifunze njia bora ya  kutokomeza   tatizo la udumavu unaotokana  na ukosefu wa lishe   bora na tayari wameisha tekeleza agizo hilo kwa kwenda  kujifunza  Njombe .

 

Amesema wananchi wa   mkoa huu  wanapaswa watambue kuwa bado wanayo kazi kubwa ya kufanya  kwani tatizo hilo lipo kwenye mkoa   hivyo wanao wajibu wakushirikiana kwa kuhakisha jambo hii la  mkakati wa kutokomeza tatizo hilo lina mgusa kila mwanamchi wa  Mkoa wa Katavi

 

Amefafanua kuwa  walipo kuwa Mkoani  Njombe  waliweza kujifunza pia nanma ya utoaji wa lishe bora kwenye  shule  na tayari   na  tayari  wamefanya  hivyo kwenye baadhi ya shule  iliwepo shule ya sekondari ya Simbwesa  kwa kuweza  kuwapatia  Ng/ombe  kwa ajiri ya maziwa .

 

Amewasisitiza   wananchi    kuzingatia  ulaji wa lishe bora  kwa kuzingatia milo  ya aina sita na pia wananchi wapende kula matunda   ya asili yanayopatikana  kwenye Mkoa wa Katavi kwani yanaweza  kuwa  na vilutubisho  kuliko matunda ya sehemu myingine .


Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi, Albert Msovela akitoa ripoti ya mpango wa haraka kupunguza udumavu

 

Baadhi ya maofisa ya serikali ya mkoa wa Katavi wakiwa kwenye uzinduzi wa kampeni ya kupunguza udumavi

 Amesema  mkoa huiu  haina sababu  yoyote  ya  kufanya washindwe kumaliza tatizo hilo kabisa  kwa njinsi ambavyo mikakati ilivyoandaliwa vizuri  na uongozi  wa  mkoa  huu.

 

Katibu Tawala wa  Mkoa wa Katavi Albart Msovela  amesema hadi sasa  juhudi balimbali zimeisha anza kufanyika  na kutekelezwa  ili  kukabiliana na changamoto hiyo ikiwa  na pamoja na kuundwakwa kamati  mbalimbali  ngazi ya Mkoa ,Halmashairi  mpaka  ngazi za  vijiji  mitaa na vitongoji

 

Kaili mbiu  ya  mkakati huo wa Mkoa wa Katavi  ni  LISHE  BORA  AFYA YAKO  ZIMGATIA  UNACHO KULA

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages