UTPC WAMPONGEZA RC KATAVI

Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa Habari Mkoa wa Katavi,Walter Mguluchuma Kushoto akitoa shukrani za UTPC kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi. 

 Na Mwandishi wetu Katavi

Muungano wa  Klabu  za Wandishi wa Habari Tanzania(UTPC) wamempongeza  Mkuu wa Nkoa wa Katavi  Mwanamvua  Mrindoko  kwa  kuweza  kuwapatia  usafiri  chama cha Wandishi wa Habari  Mkoa wa Katavi  uatako wasaidia  wandishi wa Habari  kutekeleza  majukunu yao .

Muungano wa  Klabu  za Wandishi wa Habari Tanzania(UTPC) wamempongeza  Mkuu wa Nkoa wa Katavi  Mwanamvua  Mrindoko  kwa  kuweza  kuwapatia  usafiri  chama cha Wandishi wa Habari  Mkoa wa Katavi  uatako wasaidia  wandishi wa Habari  kutekeleza  majukunu yao .

Pongezi  hizo za  UTPC zimetolewa  na  Mwenyekiti wa  Klabu ya Wandishi wa Habari wa  Mkoa wa Katavi  Walter  Mguluchuma kwa niaba ya  Mkurugenzi Mtendaji wa umoja wa klab za uandishi wa habari Tanzania [UTPC]  Keneth  Simbaya  wakati wa  Hafla fupi ya  kukabidhiwa pikipiki kwa  Klabu ya Wandishi wa Habari wa Mkoa wa Katavi iliyotolewa na  Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua  Mrindoko  .

Simbaya amesema  UTPC inapenda  kumshukuru  Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko  kwa msaada wake muhimu wa  usafiri wa pikipiki  kwa Katavi Press Club  ambayo utawahakikishia  usafiri    pia kuwa kama  chanzo cha  mapato  ya  Klabu .

 Amebainisha kuwa  msaada huu ni  kielelezo  namna  Mkoa wa Katavi  na hususani  Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko  anavyothamini kazi  za wandishi wa Habari   na kwa nsaada huu  amedhihirisha  namna  anavyothamini  nafasi muhimu  ya vyombo vya habari  katika kukuza  maendeleo  mkoani  Katavi   jamii  na  kuhakikisha  uwajibikaji  wa viongozi  katika utekelezaji wa  miradi  mbalimbali ya Serikali.

Simbaya  ameeleza kuwa  ushirikiano  kati ya Serikali  ya Serikali  za Mikoa  na  vyombo  vya  Habari  ni muhimu  kwa  mafamikio ya maendeleo  ambapo wandishi wa habari  wanweza  kuwa  washirika  wa  kusaidia  kufikisha  ujumbe  wa Serikali  kwa wananchi   kutoa maoni  ya jamii na  kuchangia  katika  kutatua changanoto  za  kijamii  kwa hivyo  msaada wake RC   Mrindoko  ni  mfano  wa  jinsi  Serikali  inavyoweza  kuimarisha  uhusiano  na vyombo  vya  habari  kwa manufaa ya wananchi .

Amesisitiza  kuwa  mfano   wake huo wa msaada kwa wandishi wa habari  unastahili  kuigwa  na viongozi  wa mikoa  mingine  hapa  Nchini  ili  vyama  vya wandishi wa habari  viendelee  kitoa  hiduma  bora  kwa wananchi   na UTPC  wanafurahia sana  na roho  hii ya ushirikiano na  wanaomba   kushirikiana kwa pamoja  katika  kufanikisha  malemgo ya  maendeleo  ya Mkoa wa Katavi na mikoa mingine pia .

Mkuu wa  Mkoa wa Katavi  Mwanamvua  Mrindoko  alisema kuwa hana  mashaka na utendaji wa kazi na wandishi wa  habari kwa  namna wanavyo utangaza mkoa  kuitia kazi mbalimbai kwenye vyombo vyao  vya habari  na       kama mkoa wataendelea kutowa ushirikiano kwa wandishi wa  habari .

Amewataka wandishi wa habari kuzingatia kufanya kazi zao kwa kuzingatia maadili ya taaluma yao katika  kuabalisha umma wa mkoa wa Katavi na Wanzania  kwa ujumla  wake   ameomba wandishi waendelee kufanya kazi kushirikiana na Serikali na wadau wengine wote.

Nae  mwandishi wa  Habari   Paul  Mathias  amemshukuru  Mkuu wa Mkoa wa Katavi kwa msaada huo muhimu ambao utawasaidia  kufanyia  shughuli za  ofisi ya Klab ya Wandishi wa  habari pia kuwafikia kwa haraka wananchi wa maeneo ya pembezoni  mwa mji pindi  kunapokuwa kumetokea matukio mbalimbali .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages