Takukuru yatoa mafunzo ya kupambana na rushwa kwa viongozi wa dini,wazee wa kimila na asasi za kiraia.

 


Na, Jackison Gerald.Katavi.

Viongozi wa dini,wazee wakimila na asasi mbalimbali za kiraia wameshauliwa kuimarisha ushirikiano wa kupambana na kuzuia vitendo vya rushwa katika kipindi hiki ambacho taifa linaelekea kufanya uchaguzi mkuu ili kuisaidia jamii kuwa na uelewa juu ya madhara ya rushwa  katika uchaguzi wa viongozi jambo litakalo saidia kupata  viongozi wenye ueledi na watakao jali haki na uajibikaji katika kuleta maendeleo kwa wananchi..

Akizungumza wakati akifungua semina kwa viongozi wa dini ,wazee wakimila na asasi mbalimbali za kiraia Naibu mkuu wa takukuru Stewart kiondo amesema ibara ya (9)h ya jamhuri ya muungano wa Tanzania inaelekeza  mamlaka za nchi , taasisi  zake na nchi kwa ujumla kuhakikisha zinaelekezwa ili kuitokomeza rushwa.




     Stewart kiondo Naibu Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Katavi akitoa mafunzo kwa viongozi wa dini ,wazee wa kimila na asasi mbalimbali za kiraia

Kiondo amesema utekelezaji wa masharti ya katiba  kuhusu kutokomeza rushwa umebainishwa katika sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa sura ya 329 na kifungu cha (7)b kikisomwa na kifungu cha (15) cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa sura ya 329 kikiitaka takukuru kuhamasisha ushiriki wa wadau ,wananchi ,taasisi na mamlaka mbalimbali katika kuondoa rushwa nchini.

Ameeleza kuwa kwa upande wa viongozi wa dini hekima na busara zitumike ili wagombea wasitumie mianya ya ununuzi  wa vifaa au uboreshaji wa miundo mbinu ya nyumba za ibada au kutoa fedha kwa ajili ya kuwavutia wananchi ili wapate fursa ya kuchaguliwa.

Amewataka kukemea kauli ya unatuachaje pindi mgombea anapokuwa amepita  katika maeneo mbalimbali ili kukabiliana na vitendo hivyo.

Kaim Katibu tawala Mkoa wa Katavi Florence chrisant amewasisitiza viongozi wa dini ,wazee wa kimila na asasi mbalimbali za kiraia kuona umuhimu wa kudhibiti vitendo hivyo kwani vinawanyima haki Watoto wa maskini wenye ndoto ya kuwa katika nyazifa mbalimbali za uongozi.

Chrisant amewaomba kudumisha amani na mshikamano kuelekea uchaguzi mkuu ili kuwezesha uchaguzi huru na wahaki utakao saidia kupata viongozi wenye ueledi na watakao jaiil haki za wananchi.



        Kaim Katibu tawala Mkoa wa Katavi akizungumza katika ufunguzi wa kikao cha mafunzo  ya kupambana na kuzuia rushwa kwa viongozi wa dini, wazee wa kimila na asasi mbalimbali za kiraia kilicho fanyika katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi. 

Akitoa mafuzo juu ya kukemea vitendo vya rushwa Afsa kutoka taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa leonard Minja amewaeleza viongozi wa dini wazee wa kimila na asasi mbalimbali za kiraia kuhamasisha jamii juu ya kuripoti vitendo vya rushwa ambavyo wenda vikafanywa na wagombea kupitia majukwaa mbalimbali ya kisiasa ,misiba na vikao mbali katika kipindi hiki ambacho inchi inaelekea katika uchaguzi.

Minja ameeleza kuwa mpaka sasa takukuru wameisha toa mafunzo  kwa viongozi wa bodaboda na makukundi mbalimbali kupitia mikutano ya hadhara.

Amewasisitiza viongozi wadini kuona umuhimu wa kupinga rushwa na kuonyesha ushirikiano wa dhati bila kuchoka kama ambavyo wemekuwa hawachoki katika kutoa elimu ya dini na mafundisho mbalimbali ya kumjua mungu.


      Viongozi wa dini ,wazee wa kimila na asasi mbalimbali za kiraia wakiwa katika mafuzo ya kuzuia na kupambana na rushwa yatakayo wawezesha kuoa elimu katika majukwaa mbalimba 

Amewaeleza kuwa takukuru itakuwa Pamoja na wao katika vita hii ya kutokomeza vitendo vya rushwa kupitia majukwaa mbalimbali ndani ya Mkoa huo.



    Sheikhe wa Mkoa wa Katavi Mashaka Kakulukulu ameishukuru  taasisi ya kuzuia na  kupambana na rushwa Takukuru Mkoa wa Katavi kwa kuwapatia elimu madhehebu ya dini ,wazee maarufu viongozi wa kimara na asasi mbalimbali za kiraia juu ya madhara ya rushwa wakati wa uchaguzi. 

Sheikh wa Mkoa wa katavi mashaka kakulukulu ameishukuru taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa takukuru kuona umuhimu wa mafunzo hayo kwa wakati muafaka ambao taifa linakwenda kufanya uchaguzi wa Rais wabunge na madiwani na yeye binafsi mafunzo hayo yamemuongezea uelewa juu ya vitendo hivyo vya rushwa na anakwenda kuwaeleza waumini kuwa chochote watakacho kifanya kutokana na rushwa madhara yake yatakuwa ni yapi .

Kwa umoja wao viongozi wadini, wazee wa kimila na asasi mbalimbali za kiraia wamesema elimu hiyo amewapa uelewa mpanda juu ya mianya ya rushwa na wanakwenda kutumia majukwaa mbalimbali kuwaeleza madhara ya rushwa ili kujenga jamii yenye uadili na inayo tambua madhara ya rushwa.

mwisho.


 

 

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages