YUMA PRE AND PRIMARY SCHOOL YACHANGIA KUINUA UBORA WA ELIMU KATAVI

Baadhi ya watoto na walimu wa YUMA PRE AND PRIMARY SCHOOL wakifurahi kwa pamoja kwenye shule hiyo mara baada ya masomo.

Wananchi wa Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wamefurahia  kuanzishwa kwa shule mpya  ya kisasa  ya YUMA  PRE   AND   PRIMARY  SCHOOL iliko  katikati ya Mji wa Manispaa ya Mpanda .

Baadhi  ya  wakazi wa Manispaa hiyo  wamesema wamevutiwa sana na miundo mbinu ya shule hiyo inayofundisha  wanafunzi  kwa masomo ya mchepuo wa masomo ya  lugha ya kingereza  kuanzia  darasa la awali .

Salome Mwanandeje Mkazi wa Mtaa wa Kawajense  ambae ni mzazi wa mwanafunzi anae  soma kwenye shule hiyo inayofundisha masomo ya mchepuo wa kiingereza ameeleza kuwa  shule hiyo ni mkombozi  katika kuinua swala zima la elimu katika Mkoa wa Katavi  na nchi  kwa ujumla.

Amebainisha kuwa imekuwa ni nadra kuona shule kama hizo zikianzishwa zikiwa na mazingira mazuri ya watoto kujifunzia na kupata elimu bora kwa watoto.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages