Na Muandishi wetu
Katavi
Wakulima wa
Tumbaku Mkoani Katavi wametakiwa
kutafuta kampuni za ununuzi wa
tumbaku watakazo ingia nazo mikataba ya kununua
tumbaku kampini zenye uwezo wa kiuchumi zitakazo walipa kwa wakati na zenye
ofisi zao ndani ya Mkoa wa Katavi
.Wito huo umetolewa na Mrajisi msaidizi wa vyama vya ushirika Mkoa wa Katavi Peter Nyakunga wakati akizungumza na wakulima wa tumbaku wa Amcos ya Kasi kwenye mkutano mkuu maalumu uliofanyika katika kijiji cha ivungwe katika Manispaa ya Mpanda .
Mrajisi msaidizi wa vyama vya ushirika Mkoa wa Katavi Peter Nyakunga akifafanua namna ya utaratibu wa Amcos juu ya kuingia Mikataba na makampuni ya ununuzi wa tumbaku wakati wa mkutano mkuu maalumu wa Amcos ya Kasi.
Amebainisha kuwa kumekuwepo na tabia ya baadhi ya Amcos kuingia mikataba ya kuuza tumbaku kwenye makampuni ambayo hayana uwezo wa kuwalipa fedha zao wakulima kwa wakati na ambazo hazina hata ofisi ndani ya Mkoa huo.Hali hii imekuwa ikiwafanya hata wakulima wakitaka
kudai haki yao au mambo
mengine mbalimbali yanayohusu zao
hilo inakuwa kwao sio
rahisi kwa kuwa baadhi ya makampuni walio ingia nayo mikataba ya ununuzi
wa Tumbaku hayana ofisi katika Mkoa huu wa Katavi .
Nyakunga amesisitiza kuwa Serikali inao wajibu wa
kuzisimamia Amcos na
kulinda masilahi ya wakulima lakini
nao wakulima wanayo haki na wajibu wa kuchagua kampuni ambayo wanataka kufanya nayo biashara
hivyo ni jukumu lao wakulima
wenyewe kuchagua kampuni wanayotaka kuingia nayo mkataba.
Wao kama serikali ni wajibu wao kuwaambia wakulima
na kuwashauri kwa kuwa huwa wameisha jua
uwezo wao wa kiuchumi wa
makampuni ambayo yanatakaka kufanya
mikataba
Alitoa
mfamo wa Kampuni ya MAGEFA ambayo
inalalamikiwa na Amcos ya
Kasi kwa kuchelewa kuwalipa wakulima wa Amcos hiyo kiasi cha dola za Kimarekani 313,261.05 wao
kama mkoa waliwashauri
wakulima kwenye mkutano juu ya kutoingia mikataba na
makampuni yasiyo na ofisi kwenye Mkoa huu lakini wakulima waligoma na sasa wamerudi kwao kuomba kuwasaidia na
wao kwa kuwa wakulima wote ni wao wanafanya
jitihada za kuhakikisha wakulima
wanalipwa madai yao .
Amefafanua kuwa sio kwamba ni Serikali ya Mkoa tu inayofatilia madai hayo ya wakulima hao ni mpaka Waziri wa Kilimo anajua na ndio maana anafuatilia kwa karibu sana kwa kuwa anatambua kulitokea changamoto ya makampuni mengi kununua tumbaku nje ya yale makisio yao .
Mkulima Cristopher Januari alimuomba
mrajisi msaidizi aendelee kuwasaidia kama ambavyo amekuwa
akiwasaidia kwa kuwa yeye ndie mlezi wao na baba yao wa Amcos zote katika Mkoa
wa Katavi na pia aendelee kufuatilia walipwe fedha wanazo dai.
Mwenyekiti wa Amcos ya Kasi Deis Maganga amesema
Mrajisi msaidizi amekuwa bega kwa bega na wakulima hata wanapokuwa kwenye changamoto amekuwa nao
na ndio maana hata hivi karibuni alikwenda kufuatilia madai yao ya fedha za
wakulima wanazo dai .
Maganga amesema mrajisi msaidizi wa mkoa wa Katavi wakulima
wote ni wake na watoto wake hivyo wanapokuwa wamekosea awasamehe kwani
wamekuwa wakitoa mambo yao nje kabla ya wao kuwa wamekaa hivyo ni sawa na wao kudai haki bila kufuata sheria.
Baadhi ya wakulima wa Kasi Amcos wakiwa kwenye mkutano huo wakifuatilia kwa makini
MWISHO