RC KATAVI AMSHUKURU RAIS SAMIA KWA JITIHADA YA KUTATUA CHANGAMOTO ZA BARABARA

 

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko [katikati]akitoa maelekezo ya ujenzi wa Daraja la Katuma eneo la sitalike alipotembelea na kujionea mwenendo wa ujenzi huo.
Na Walter Mguluchuma-Katavi

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua  Mrindoko amemshukuru  Rais Dk  Samia Suluhu Hassan kwa  jitihada kubwa sana  za kuhakikisha kwamba  katika kipindi chake cha utawala  anaondoa changamoto  mbalimbali za  barabara zinazouunganisha Mkoa wa Katavi na Mikoa mingine na barabara za ndani ya mkoa.

Muonekano wa Daraja la Katuma sitalike linalounganisha Mkoa wa Katavi na Rukwa ambalo ujenzi wake umefikia asilimia 83%

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua  Mrindoko amemshukuru  Rais Dk  Samia Suluhu Hassan kwa  jitihada kubwa sana  za kuhakikisha kwamba  katika kipindi chake cha utawala  anaondoa changamoto  mbalimbali za  barabara zinazouunganisha Mkoa wa Katavi na Mikoa mingine na barabara za ndani ya mkoa

Pongezi hizo amezitowa  wakati alipokuwa  akikagua  utekelezaji  wa ujenzi wa Daraja la Sitalike lenye utefu  wa  Mita 55 linalojengwa  kwa  Zaidi ya Bilioni 9.1  linalouunganisha Mkoa wa Katavi na Mkoa wa Rukwa  pamoja na Hifadhi ya Taifa ya Katavi ambalo  limekuwa na changamoto ya muda mrefu wakati wa kipindi cha masika

Mrindoko amesema  Rais  Dkt  Samia Suluhu  Hassan  amefanya kazi kubwa katika kipindi  cha uongozi wake  kuhakikisha anaondoa miundo mbinu mbali ya  barabara inayouunganisha Mkoa wa Katavi  na Mikoa mingine .

Amebainisha kuwa   tunafahamu  kuwa mkoa huu umetoka mbali katika  maswala  ya upatikanaji wa barabara kuu  na wanaendelea kwa kasi kubwa sana  kwa ujenzi wa barabara zito zinazounganusha mkoa huu na mikoa mingine  kuwa zinapitika katika kipindi chote cha mwaka  mzima .

Ameeleza kuwa  daraja hilo    lilikuwa  na adha kubwa hasa wakati wa kipindi cha mvua  kama ambazo zilitokea hivi karibuni mwaka 2024 wananchi walikwama  na kulazimika kulala porini ndani ya hifadhi ya Katavi baada ya daraja  sasa kufunikwa na maji kwa muda wa siku kumi na nane,(18)

Mrindoko amefafanua kuwa ndio maana ametoa  shukurani kwa  Rais  Samia  ametowa fedha kwa kupitia  Benki ya Dunia  kwa lengo la kuhakikisha  daraja la uhakika zaidi linapatikana  katika barabara hiyo muhimu.

Adha  amemshukuru  mkandarasi  kampuni ya M/S Mselem Civil  Engineering  and  Buildimg  Contractors Limited  JV  Mbuyas Contractors Company Limeted kwa kazi  walioifanya ya ujenzi wa baraja hilo hali ambayo inaonyesha  litakamilika  muda si mrefu na litaanza kitumika .

Meneja wa Tanroads  Mkoa wa Katavi Mwandisi  Martin Mwakabende amesema  ujenzi wa  daraja hilo ni   utekelezaji wa ahadi  za Rais.

Ambapo  ujenzi huo unagharimu  kiasi cha Shilingi 9,106,238,961.00  na kazi  za  ujenzi  zinaendelea  utekelezaji wake hadi sasa imefikia asilimia 83 huku muda wa utekelezaji ukiwa umefikia  muda wa miezi 11 kati ya miezi 12.

Mkurugenzi wa Kampuni ya M/S  Mselemu Civil  Engineering Nassor Mselemu amesema wanatalajia kukamilisha ujenzi kwa muda uliopangwa licha ya wao kuwa  wameomba waongezewe  mwezi  mmoja wa muda wa ziada.                                                   

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages