VIONGOZI WAWILI AMCOS MIKONONI MWA TAKUKURU KATAVI KWA MATUMIZI MABAYA YA MADARAKA



Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Katavi,Christopher Nakua.
Na Walter Mguluchuma KTPC,Katavi.

Taasisi ya kuzuia na Kupambana na Rushwa  ( TAKUKURU)  Mkoa wa Katavi  kwa kushirikiana na ofisi  ya Taifa ya  Mashitaka  wanakusudia  kuwafikisha Mahakamani Viongozi watatu  wa zamani  wa Mishamo  Amcos  Ltd  kwa kosa la kutumia vibaya madaraka   mabaya kichume  na kifungu  cha 31 cha sheria ya kuzuia na  kupambana na Rushwa Na.11 ya  mwaka 2007.

 Mkuu wa Takukuru  wa Mkoa wa Katavi Cristopher  Nakua   amewataja viongozi hao wanaotarajiwa kufikishwa Mahakamani ni  Pridance  Anacredo Mark  ambae mpaka wakati uchunguzi wa kosa hilo unapofanyika alikuwa ni  Mwenyekiti wa Mishamo Amcos Ltd na   Valantho  Wiliam Gataro  ambae wakati huo wa mwaka 2016 alikuwa ni Meneja wa   Mishamo Amcos  Ltd.

 Nakua ameeleza kuwa  viongozi hao wote wawili  wakiwa kwenye  majukumu yao utekelezaji  kama viongozi  walitumia vibaya  madaraka yao  kwa kuidhinisha mkopo  wa fedha kiasi cha  Tshs,4,000,000 kwa    Freddy  Moses ambae hakusitahili  kupewa  mkopo huu kwa kuwa  hakuwa mwanachama wa Mishamo Amcos Ltd.

 Watuhumiwa hao kwa kufanya hivyo  walikiuka  sheria  na kanuni  za ushirika  na hata  katika chama hicho  zinazotaka  mikopo  ya fedha za chama sharti  zitolewe kwa wanachama pekee.

Uchunguzi wa  Takukuru   ulibaini  kuwa  Freddy Moses mwaka 2014 kupitia  Kampuni yake  ya Mtuka  Environmental Rehabilitation Compny ilisaini mkataba  na Mishamo Amcos Ltd  kwa ajiri ya kuotesha miche  484,924.

 Amesema hivyo  kwa kupitia ukaribu  na watuhumiwa  wakati wa kutekeleza mradi  huu aliweza kukopeshwa  kiasi  cha  fedha kinyume na utaratibu .

Amefafanua  kuwa  kwa mujibu  wa kifungu kilichotajwa  watuhumiwa hao  walikiuka  sheria  katika utoaji wa  mkopo  na kusababisha  Freddy Moses kujinufaisha  na kupata manufaa  ya faida  asiyo  kuwa anasitahili .

 Nakua ameeleza kuwa  kumekuwa na  tuhuma nyingi  zinazohusu  vyama mbalimbali  vya ushirika  katika Mkoa wa Katavi  na nchi kwa ujumla  na tuhuma nyingi  zimejikita zaidi  kwenye matumizi mabaya ya madaraka  na ubadhirifu wa fedha  za vyama .

  Hivyo  Takukuru Mkoa wa Katavi  wanaendelea  kufanya uchunguzi  dhidi ya tuhuma hizo  na uchunguzi  ukikamilika  hatua  stahiki  za  kisheria  zitachukuliwa .

 Ametowa  shukuru kwa wandishi wa Habari wa Mkoa wa Katavi  kwa ushirikiano wao mkubwa  katika mapambano dhidi ya Rushwa wanaoutowa kwa Taasisi hiyo 

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages