WAKAMATWA NA VIPANDE VYA MENO YA TEMBO 16


Baadhi ya meno ya Tembo yaliyokamatwa na jeshi la polisi katika mkoa wa katavi 

Na  Walter  Mguluchuma, Katavi .

Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Askari wa Hifadhi ya Taifa  ya  Katavi  wamefanikiwa kuwakamata watuhumiwa wanne wakiwa na meno ya Tembo vipande 16   ambavyo ni sawa na tembo saba hai  katika  matukio mawili tofauti .

Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Askari wa Hifadhi ya Taifa  ya  Katavi  wamefanikiwa kuwakamata watuhumiwa wanne wakiwa na meno ya Tembo vipande 16   ambavyo ni sawa na tembo saba hai  katika  matukio mawili tofauti .

Kaimu   Kamanda wa Jeshi la Polisi  Mkoa wa Katavi  Kaster Ngonyani ameeleza kuwa watuhumiwa hao wamekamatwa kufatia  msako  mkali uliofanywa na Askari wa jeshi la polisi  kwa kushilikiana na Askari wa Hifadhi ya Taifa ya Katavi  mara baada ya kuwa wamepata taarifa juu ya watu hao kujihusisha na  biashara halamu ya nyara za serikali.

Katika tukio la kwanza  lilitokea  katika  maeneo  ya Mtaa wa Kwalakwacha  Kata ya Nsemlwa Manispaa ya Mpanda  mtuhumiwa  Juma  Malongo (47) Mkazi wa Mtaa wa Kozazi Manispaa ya Mpanda  alikamatwa akiwa na vipande kumi  vya  meno ya tembo

Mtuhumiwa huyo  alikuwa ameficha meno ya  tembo   katika chumba  alichokuwa akiishi  kwa kwenye mfuko wa  salifeti .

Kaimu  Kamanda  Ngonyani amesema   tukio jingine lilitokea huko  maeneo ya  Itunya  Tarafa ya Kapalamsenga Wilaya ya  Tanganyika  ambapo watuhumiwa  watatu  ambao  Edesi  Maridadi (62)  mkazi wa  Kalia Kabwe  Wilaya ya Nkasi Riukwa , Silas  Maiko(19) na  Julius  Msumeno wakazi wa  Kalia  Kabwe walikamatwa wakiwa na  vipande sita vya mano ya tembo .

Amesema kuwa watuhumiwa hao walikamatwa na nyara hizo za serikali wakiwa wamehifadhi ndani ya nyumba yao waliyokuwa wakiishi kwa lengo la  kutafuta mteja ili waweze kufanya biashara haramu.

Aidha  katika eneo la  Kaburiwazi  ndani ya pori  la akiba  Rukwa  wilaya ya Mlele  Mkoa wa Katavi  wamekamatwa watuhumiwa watano wakiwa na  silaha aina ya Gobole mbili  pamoja na nyama  ya pori.

Amewataja watuhumiwa hao kuwa ni  Pius Mbalamwezi  Edward  John , Good frey   Mwaka ,Crispin George na  Gelad Mashamba  wote wa kazi wa Kijiji  cha  Muze  Wilaya ya Sumbawanga Mkoani Rukwa .

Mhifadhi  Mwandamizi, Kaimu Mhifadhi  ya Hifadhi ya Taifa ya Katavi  Francis   Kone  Makaranja  amesema kuwa  wanyama hao wamekuwa wakiuawa kwenye maeneo ya nje ya Hifadhi ya Taifa ya Katavi.

Amefafanua kuwa  wamekuwa wakileta nyara hizo za serikali kwa lengo la kuja kuzificha na kutafuta soko lakini kutokana na ushirikiano mkubwa wa vyombo vya ulinzi na usalama vinavyoshirikiana na askari wa  Hifadhi ya Katavi  wameweza kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa hao .

Makaranja amewaonya watu  wote ambao wanajihusisha na  swala la  ujangili waache mara moja kwani  watumbue kuwa   ulinzi ulipo ndani na nje ya  Hifadhi ya  Taifa ya Katavi ni kubwa

Watuhumiwa hao bado wanaendelea  kuhojiwa   na mara uchunguzi utakapokuwa umekamilika  watafikishwa mahakamani ili wakajibu tuhuma  zinazo wakabili .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages