MANISPAA YAPOGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI

 

Msitahuki Meya wa Manispaa ya Mpanda Haidary Sumry akifungua Kikao cha Baraza maalumu la Mdiwani la kujadili taarifa za Mkaguzi mkuu wa Hesabu za Serikali zinazoishia June 2022.

Na Walter Mguluchuma 

Mpanda.

Manispaa ya  Mpanda  Mkoani  Katavi imepongzwa kwa kuwa ni miongoni mwa  Halmashauri hapa Nchini kwa kupata hati safi  katika taarifa iliyotolewa na   mkaguzi Mkuu wa Serikali kwa mwaka wa fedha 2021 na 2022 kutokana na utendaji kazi mzuri   unaofanywa na Halmashauri hiyo .

Madiwani wa Manispaa ya Mpanda wakiwa kwenye baraza maalumu la kujadili taarifa za Mkaguzi na Mkaguzi  mkuu wa Hesabu za Serikali [CAG]

Manispaa ya  Mpanda  Mkoani  Katavi imepongzwa kwa kuwa ni miongoni mwa  Halmashauri hapa Nchini kwa kupata hati safi  katika taarifa iliyotolewa na   mkaguzi Mkuu wa Serikali kwa mwaka wa fedha 2021 na 2022 kutokana na utendaji kazi mzuri   unaofanywa na Halmashauri hiyo .

Pongezi  hizo zimetolewa kwa nyakati tofauti wakati wa kikao  maalumu cha  Baraza  la Madiwani  lililo kutana kwa ajiri ya kujadili taarifa ya mkaguzi  mkuu wa Serikali iliyoishia June 2022 kikao hicho cha Baraza la Madiwani kimefanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Mpanda na kuongozwa namstahiki  Meya wa Manispaaya Mpanda  hiyo Haidari Sumry .

 Akiwatubia wajumbe wa Baraza hilo la Madiwani   Katibu  Tawala wa Mkoa wa  Katavi Hassan    Abas Rugwa ameeleza kuwa  hayo wanayo yashuhudia  kwenye Manispaa ya kupata hati safi inatokana na ufanisi wa muunganiko wa Madiwani    pamoja na wataalamu .

Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa ambae pia ni Mkuu wa Wilaya ya Tangayika onesmo Buswelu akilihutubia baraza maalumu la Mdiwani lililokuwa linapitia taarifa za Mdhibiti na mkaguzi mkuu wa Hesabu za serikali

Amebainisha kuwa ni  madiwani ndio wenye jukumu la kuisimamia  Halmashauri  hivyo hakuna budi  kuwapongeza na kuwatia moyo  ili waendelee kuisimamie  Manispaa  iendelee kufanya vizuri

Rugwa amewataka    waendelee kusimamia pale waliposimamia  na waendelee kubuni mikakati mipya  na nzuri zaidi ya kuweza kuisimamia Halmashauri  ili Kuyafikia malengo ndani ya Halmashauri.

  Amefafanua kuwa pamoja na mafaniko hayo   zipo baadhi ya changamoto  kwenye baadhi ya maeneo ambazo zimewafanya wafike hapa kwa ajiri ya kujadili changamoto hizo chache  na wanao uwezo wa kufanya hoja hizo  hazijitokezi tena kwa kuwa  uwezo huu upo ndani  ya Halmashauri yenyewe .

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph akifatilia kwa Makini taarifa za Mkaguzi mkuu wa hesabu za wakati wa kikao cha baraza maalumu la Madiwani halmashauri ya Manispaa ya Mpanda

Meya wa Manispaa ya Mpanda  Haidari  Sumry ameeleza kuwa  hadi June 2022  walikuwa wamepokea hoja 55 za kutoka kwa GAG hata hivyo wameweza  kujibu  hoja   30 na sasa wamebakiza hoja 25.

Amesema  watahakikisha wanaendelea kufanya kazi kwa kushirikiana  karibu na uongozi wa  Serikali wa Wilaya  na Mkoa na wako  tayari kuendelea kupokea ushauli ili waendelea  kufanya  vizuri katika usimamizi wa fedha na miradi ya maendeleo .

Mkuu wa  Wilaya ya Mpanda Jamira Yusuph  amesema kuwa ni faraja kwa Halmashauri hiyo kuweza kupata hata safi  hali  hii inaonyesha kuwa kuna kazi kubwa imefanywa kwenye Manispaa ya Mpanda.

Mwakilishi wa  Mkuu wa Mkoa  kwenye kikao hicho ambae ni Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika  Onesmo  Busweru  amewataka wafanye kazi kwa kuzingatia  sheria na taratibu  za manunuzi ili kuepukana  hoja za CAG ambazo zinaweza kujitokeza .

Amewasisitiza  wakusanye  mapato kwa halali  na kwa weledi mkubwa   ili waweze kufikia malengo waliojiwekea  na kuweza kuwahudumia wananchi kwa kuwatatulia changamoto zao .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages