RUWASA YAJA KIVINGINE UTOAJI HUDUMA KWA WANANCHI

 

Kaimu Meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini Ruwasa Wilaya ya Mpanda Mhandisi Christian Mpena akizungumzia mfumo wa kulipia Huduma ya Maji kwa wakazi wa Vijijini kupitia mfumo wa luku.

Na Paul Mathias,Mpanda.

Wananchi katika Kijiji cha Kanoge Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi wamesema kuwa serikali kupitia Wakala wa Maji na usafi wa Mazingira Vijijini Ruwasa Wilaya ya Mpanda Kuja na Mfumo wa kulipia huduma ya Maji kwa Luku utasaidia ukusanyaji wa Mapato kwa serikali.

Moja ya Mita ya Maji iliyofungwa katika mfumo wa luku  katika kijiji cha Kanoge ambapo wananchi watalipia huduma ya Maji katika mfumo wa Luku kadri ya mahitaji yao

Wananchi katika Kijiji cha Kanoge Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi wamesema kuwa serikali kupitia Wakala wa Maji na usafi wa Mazingira Vijijini Ruwasa Wilaya ya Mpanda Kuja na Mfumo wa kulipia huduma ya Maji kwa Luku utasaidia ukusanyaji wa Mapato kwa serikali.

Wananchi hao wamebainisha hayo kijijini hapo Baada ya kufikiwa na chombo hiki ili kufahamu namna mfumo huu utawasaidia wananchi na serikali katika kupata kukusanya mapato na huduma ya maji kijijini hapo.

Akisa Linus Mkazi wa kijiji cha Kanoge amesema kuwa wanaishukuru serikali kwa kuja na Mfumo wa kulipia Maji kwa njia ya Kadi ambayo itaepusha usumbufu wa upatikanaji wa huduma ya maji na kusaidia Mapato ya serikali.

Wakazi wa Kijiji cha Kanoge wakiendelea kupata huduma ya Maji kupitia mfumo wa lipa kabla ambao ambao umeletwa na Ruwasa kwa lengo la kukusanya mapato na kuepusha upotevu wa Maji 

‘’tunaipongeza serikali kwa kutuletea huu mfumo wa Kadi hii ya Maji sisi kama wananchi itakuwa na unafuu kwa sasabu kila mtu atakteka maji kwa muda anaoutaka na itatusaidia katika kuingiza kipata kwenye serikali tunaiishuru serikali na Ruwasa’’mesema akisa

Kwa upande wake Abikolimana Yusuph Mkazi wa kijiji cha Kanoge amesema Mara baada ya Serikali kuleta Mradi huo kupitia Ruwasa baada ya muda walileta Mfumo wa kisasa wa kulipia huduma ya Maji kupitia kadi kwa mfumo wa Vocha.

‘’Abilikomama anasema unaweka Pesa kwenye ile kadi halafu ndo unaenda kununua kulipia maji pale ukiweka kadi hiyo kwenye Mita Maji yanatokana kulingana na kiwango ulicholipia’’

Elisha Chagula mwenyekiti wa Kamati za Watumiamaji katika Kijiji cha Kanoge na Litapunga ameiomba serikali kuendelea kuweka mifumo hiyo kwenye maeneo mengine kwakuwa ni lafiki kwa Mwanachi na unaisadia serikali ukusanyaji wa Mapato.

huu mfumo ni mzuri sana ukiendelea kwenye maeneo menginine utafanya wateja wetu kulipia huduma hii kwa haraka kwa kadri wanavyo hitaji maana mfumo huu hauna usumbufu wa kumuweka muuza maji kwenye kituo mfumo utajiendesha wenyewe ameeleza chengula.

Kaimu Meneja wakala wa maji na usafi wa Mazingira Ruwasa Wilaya ya Mpanda Mhandisi Christian Mpena amesema Wilaya ya Mpanda imepokea mita za luku za maji tatu ambazo zimefungwa katika Kijiji cha Kanoge Sokoni,Kituo cha afya Kanoge na Shule ya Msingi Stalike.

‘’natoa shukurani za pekee kwa serikali ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania kwa Mpanda tulipokea [Water miter Pre Paid] mita za luku za maji tatu ambazo zimefungwa shule ya msingi Stalike,Kituo cha afya kanoge na kijiji cha Kanoge sokoni’’amesema Mpenda.

Moja ya Mita ya maji iliyofungwa katika Kituo cha Afya Kanoge ambayo inatumia Mfumo wa Luku kwa watuamiji wa Maji kulipia kabla ya kupata huduma hiyo 

Mpena amesema kuwa mfumo huo utaisadia sana serikali kukusanya Mapato yake kwakuwa watumia Maji watakuwa wanalipia huduma hiyo moja kwa moja kwa njia ya Luku kulingana na mahitaji yao.

Katika hatua nyingine ameawaomba wananchi kuendelea kuitunza miundo mbinu hiyo ambayo inaletwa na serikali kwenye maeneo yao.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages