| Mwenyekiti wa Bodaboda Mkoa wa Katavi Issack Joseph akizungumnza na waandishi wa habari |
Mwenyekiti
wa bodaboda Mkoa wa Katavi Isaack Joseph amewataka Madreva kuwasajili bodaboda
waliopo kwenye vituo vyao mbalimbali ili kuepuka vitendo vya uharifu
vinavyofanywa na baadhi ya watu ambao siyo Madreva bodaboda.
Mwenyekiti wa bodaboda Mkoa wa Katavi Isaack Joseph amewataka Madreva kuwasajili bodaboda waliopo kwenye vituo vyao mbalimbali ili kuepuka vitendo vya uharifu vinavyofanywa na baadhi ya watu ambao siyo Madreva bodaboda.
Akizungumza
na Waandishi wa habari Joseph amesema kuwa hivi karibuni pamekuwa na baadhi ya
waendesha pikpiki ambao hujivisha taswira za dereva bodaboda na kufanya uharifu
huku wakijitambulisha kuwa bodaboda huku wakiwa hawana usajili Rasmi.
’’
sisi kama viongozi wa bodaboda Mkoa wa Katavi,tunataka viongozi wote wa Kanda
zote zinazounda Mkoa wetu wa Katavi kuhakikisha kuwa bodaboda wote
wanaopokelewa katika vituo hivyo wawe na nyaraka zote za kuwatambulisha yaani
kutika serikali za Mitaa pamoja na nyaraka kutoka katika uongozi wa bodaboda
mkoa’’amesema Joseph
Aidha mwenyekiti huyo amesema kuwa wao kama
bodaboda wataendelea kuwa mabalozi wa kuhubiri umoja amani na mshikamano kwa
wananchi wa mkoa wa Katavi.
Jouachimu
Ndile Mwendesha bodaboda Mkoa wa Katavi amesema wataendelea kutoa taarifa kwa
baadhi ya bodaboda ambao wamekuwa na tabia ya kuingia kwenye kazi hiyo pasipo
kufuata utaratibu na kujihusisha na vitendo vya uharifu.
“Kwakweli
alicho kisema mwenyekiti wetu ni cha msingi na cha kuzingatia ni jambo la
msingi kuwatambua wote wanaofanya kazi hii kwani kuna wengine malengo yao siyo
mazuri ni kutuchafua sisi wengine ambao hatujihusishi na uharifu’’amesema Ndile
Uongozi wa Bodaboda umeahidi kuhakikisha unashirikiana vyema na serikali ili kuhakikisha amani iliyopo mkoa wa Katavi na Taifa zima kwa ujumla inaendelea kudumu kwani bila amani basi hakuna maendeleo yoyote yatakayofanyika.