BODI YA TUMBAKU YAONYA MAKAMPUNI KUCHELEWESHA MALIPO YA WAKULIMA

Mkurugenzi mkuu wa bodi ya Tumbaku Tanzania Stanley Mnozya akielezea mkakati wa bodi ya Tumbaku kwa makampuni ya ununuzi wa zao hilo .

 Na Walter Mguluchuma-Katavi

Mkurugenzi  Mkuu wa Bodi ya Tumbaku Tanzania    Stanley  Mnozya     ameyaagiza  makampuni  yote yanayonunua Tumbaku kwa wakulima kuhakikisha  yanafuata kanuni na taratibu ya kulipa fedha za wakulima kwa wakati huku akionya kampuni ambazo zitashidwa kufanya hivyo zitachukuliwa hatua kali za kisheria.

Mkurugenzi  Mkuu wa Bodi ya Tumbaku Tanzania    Stanley  Mnozya     ameyaagiza  makampuni  yote yanayonunua Tumbaku kwa wakulima kuhakikisha  yanafuata kanuni na taratibu ya kulipa fedha za wakulima kwa wakati huku akionya kampuni ambazo zitashidwa kufanya hivyo zitachukuliwa hatua kali za kisheria.

Hatua hiyo ya Bodi ya Tumbaku  imechukuliwa kufatia kuwepo kwa malalamiko kwa baadhi ya Amcos  hapa nchini ikiwepo KASI AMCOS ya  Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi  kuchelewechewa  malipo yao na  baadhi ya Makampuni .

Mnozya  amesema  alipokuwa Katavi alikutana na kesi kwamba  chama cha Msingi Kasi kilikuwa  hakija lipwa fedha zao kiasi cha Dolla  Zaidi ya 312 000 na kampuni moja ya ununuzi wa zao la Tumbaku .

Kufatia changamoto hiyo yeye Mkurugenzi Mkuu wa bodi ya Tumbaku aliwahidi wakuluma hao kuwa atashughulikia changamoto yao  na tayari wakulima hao kulipwa fedha zao zote  na kufanya  Mkoa wa Katavi wakuluma wake wote kulipwa kiasi cha shilingi Bilioni   120 na kwa sasa hakuna mkulima ambae anadai fedha yoyote ile .

Mnozya  ameziagiza Kampuni zote zinazo nunua zao la Tumbaku hapa nchini   kuhakikisha zinafuata sharia  kanuni na taratibu zinapokuwa zimenunua tumbaku ya wakuluma    zilizopo  na wasichelewesha malipo ya wakuluma kufanya hivyo ni uvujanji wa sharia zinazosimamia zao hilo .

Ameyaonya makampini yote yanayonunua Tumbaku hapo nchini kwa msimu ujao yatakayo jaribu kuwachelewesha wakuluma hatua kali sana  za kisheria zitachukuliwa dhidi yao .

Mnozya amesisitiza kuwa kitendo cha kuwachelewechea malipo  ni kuwahuhumu wakuluma  kwani mkulima amelima ilia pate  fedha  aweze kujenga nyumba .kulipia ada za watoto shule na pia grarama za matibabu na mahitaji mengine mbalimbali  ya  maendeleo .

Hivyo unapomcheleweshea unamrudisha nyuma  maendeleo yake  hivyo makapuni yahakikishe yanajipanga vizuri kuona namna  ya kuwalipa wakuluma kwa wakati .

Amewaasa wakulima  wauze tumbaku  pindi Bodi ya Tumbaku inapokuwa imetangaza kuanza masoko  mwezi wan ne au watano kwani kipindi hicho tumbaku  inakuwa na uzito na ubora na wakuluma wanapata fedha za kitosha .

Lamack Mbuza  mkulima wa Amcos ya Kasi amesema kwa msimu huu wamepitia katika kipindi kigumu sana  kufutia kampini ya Magefa kuchelewa kuwalipa fedha zao   hadi  jitihada  kubwa zilizofanywa na Mkurugenzi wa Bodi ya Tumbaku na timu yake ndio wameweza kulipwa hivi karibuni fedha zao zote ,

Makamu Mwenyekiti wa Amcos ya Kasi Gerald Kipanta  ameyaomba makampuni yanayonunua zao  la Tumbaku kuwa na utaratibu wa kuwalipa wakulima mapema .                                                 

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages