WAKULIMA WASHUKURU BODI YA TUMBAKU KWA KUTATUA CHAMGAMOTO YA MALIPO YAO.

Baadhi ya Wakulima wa Kasi Amcos wakiendelea na shuhguli za kilimo cha Tumbaku.

 Na Mwandishi wetu-Katavi

Wakulima  wa zao la Tumbaku wa Amcos ya KASI  katika  Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi  wameishukuru Bodi ya Tumbaku Tanzania  kwa  kuwasaidia kuweza kulipwa  fedha zao Zaidi ya Dolla 312,000 ambazo  walikuwa wanadai mrefu kutoka kampuni ya ununuzi wa Tumbaku ya Magefa.

Wakulima  wa zao la Tumbaku wa Amcos ya KASI  katika  Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi  wameishukuru Bodi ya Tumbaku Tanzania  kwa  kuwasaidia kuweza kulipwa  fedha zao Zaidi ya Dolla 312,000 ambazo  walikuwa wanadai mrefu kutoka kampuni ya ununuzi wa Tumbaku ya Magefa

Wakizungumnza na Gazeti hili wakulima hao wameeleza kuwa kilio cha kutolipwa fedha zao za msimu wa Tumbaku uliomalizika mwaka huu kilikuwa cha muda mrefu tangu walipo maliza masoko yao mwezi wa Julai.

Lameck Mbuza Mkulima wa Kasi Amcos amesema wao kama wakulima wamepitia kipindi kigumu kabla ya malipo hayo kufanyika walikuwa wameingika madeni mitaani lakini baada ya malipo kufanyika wameweza kurejesha.

lameck Mbuza Mkulima wa Kasi Amcos akielezea namna malipo yao ya Tumbaku yalivyosaidia kubadilisha maisha yao.

Hali hiyo imewafanya waendelee na shughuli za kilimo cha Tumbaku kwa msimu huu kwani pembejeo zote zipo za kutosha na zimefika kwa wakati  kwa hiyo watahakikisha wanalima kwa nguvu.

‘’tunamshukuru Mkurugenzi wa bodi ya Tumbaku Tanzania kwa kufika mkoa wa Katavi pindi tulipokua tunadai tunaamini kufika kwake kumeleta msukumo wa kufanyika kwa malipo yetu yaliyokua yamekwama’’ amesema Mbuza.

Gerald Kipanta Makamu mwenyekiti wa Kasi amcos akiishukuru serikali kwa kuwalipa fedha zao Tumbaku.
Ameyaomba Makampuni yanayoingia mkataba wa ununuzi wa Tumbaku kwenye vyama vya msingi kuharakisha malipo pindi wamapo kuawamenunua Tumbaku ya wakulima na kuwafanya wakulima kuwa na ari ya kulima kwani nao wanatamani kutembelea Magari na kuishi maisha mazuri yenye uchumi imara.

Paul Yahila Mkulima wa Kasi Amcos ametoa ushauri kwa makampuni ya ununuzi  wa Tumbaku kufata sheria na taratinu ili kuepusha kuwepo kwa changanoto ya wakulima kucheleweshewa malipo yao.

Amebainisha kuwa kilimo cha Tumbaku wanakianza mwezi Agosti lakini changamoto inatokea pale malipo yanapochelewa huwa wanaumia sana hali ambayo huwapelekea kwenda mitaani na kuchukua mikopo isiyorasmi ambayo hua na riba kubwa.

‘’Msimu huu tumelipwa mwezi huu wa Novemba na tulianza maandalizi ya kilimo mwezi wa Agosti hali hii hua inawavunja nguvu wakulima’’amesema Yahila.

Joseph Yamala amesema kabla ya malipo ya Tumbaku walipitia maisha magumu kwenye kuendesha maisha yao huku akishukuru baada ya malipo mambo yamekaa sawa na wanaendesha maisha yao kama kawaida.

Katika hatua nyingine amewashukuru viongozi wa Chama kikuu cha Ushirika Mkoa wa Katavi Latcu na Mlajisi Msaidizi Peter Nyakunga kwa jitihada mbalimbali walizozifanya.

Kwa upande wake Makamu mwenyekiti wa Kasi Amcos Gerald Kipanta ametoa shukrani za pekee mkurugenzi wa Bodi ya Tumbaku Tanzania kwa msukumo mkubwa alioufanya mpaka wakulima wamelipwa fedha zao na sasa wengine wanenunua viwanja ,Bajaji,Pikipiki na wengine wanasomesha watoto wao waliokuwa wamekwama kuwapeleka shule kwa kukosa pesa.

Kipanta amesema wakulima wao wote wamelipwa fedha zao Zaidi ya Dolla 312,000 ambayo ni malipo ya zao hilo kwa wakulima kwa msimu wa kilimo wa 2024/2025.

Stanley Mnozya Mkurugenzi wa Bodi ya Tumbaku Tanzania ameagiza makampuni yote yanayonunua Tumbaku kuhakikisha wanafanya malipo ya wakulima kwa muda muafaka kwa mujibu wa sharia.

Mnozya ameeleza kuwa kwa sasa katika mkoa wa Katavi wakulima wote wa zao hilo wamelipwa fedha zao kiasi cha zaidi ya Dolla Milioni 47 sawa na Zaidi ya Bilioni 120 hivyo kwa sasa hakuna wakulima kwa mkoa wa Katavi wanaodai fedha za msimu uliopita.

Amebainisha kuwa alipokuwa Mkoa wa Katavi alikutana na malalamiko ya wakulima wa chama cha ushirika cha Kasi na kuwaahidi kwenda kufatilia changamoto yao ambayo aliishughulikia na wakulima wamelipwa fedha yao waliokuwa wanadai.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages